Promote your business for free grow your business for life you don't need to spend more money anywhere.

THIS BLOG IS SPONSORED BY AHADIWAY ,ADVANTAGES FOR JOINING AHADIWAY BOON CAREER (ABC) CHAPTER = Employment opportunities within and outside the country. , Job experience , Self -employment , Field stations, part time jobs and chances to be trained.

Tuesday, February 1, 2011



THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT - BEYOND THE ORDINARY - NATURALLY'
Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Nawasihi kila mmoja wetu ajiheshimu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya GLOBU YA JAMII, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoelezwa vi

waliosoma shule ya sekondari ya malangari kukutana jijini dar



KUTAKUWA NA KUSANYIKO LA WATU WOTE TULIOSOMA SHULE YA SEKONDARI MALANGALI KWA AJILI YA KUFAHAMIANA NA KUJADILI MASUALA YA PAMOJA NA MAENDELEO.


KUSANYIKO LITAKUWA TAREHE 5/2/2011 SAA 9 JIONI CHONYA INN (RIVER SIDE)MBELE KIDOGO YA LANDMARK HOTEL UBUNGO, UKITOKEA UBUNGO. TAFADHALI TUJULISHANE WENGINE. MAWASILIANO PIGA 0787525396

Tanzania receives ALMA award of Excellence in Addis Ababa



Tanzania yesterday received the First African Leaders Malaria Alliance award of excellence for its efforts in combating Malaria in the country.In the picture The United Nations Secretary General Ban-ki-Moon hands over the award to President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete in Addis Ababa Ethiopia while the chairman of the AU Commission Jena Ping(centre) looks on.(photo by Freddy Maro)


dkt john pombe magufuli awasha moto dar leo




Waziri wa Miundombinu, Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mthamni Mwandamizi wa Wilaya ya Kinondoni, Einhard Chidaga, wakati alipokuwa katika ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Barabara ya Ubungo Maziwa, inayotokea Kigogo, wakati wa ziara hiyo iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam, wakati huo huo Waziri huyo ametoa siku tano kwa Meneja wa Mkoa kubomoa ofisi yake iliyopo Ubungo, ili iwe mfano kwa raia wengine wanaotakiwa kupitiwa na zoezi hilo la ubomoaji ili kupisha upanuzi wa Barabara na mradi wa Magari yaendayo kasi. Picha na mdau Muhidin Sufian.

maiti za vichanga 10 vyaokotwa jalalani dar leo



Miili ya vichanga 10 vilivyokutwa vimetupwa katika jalala kwenye nyumba moja iliyo jirani na makaburi ya Mwananyamala, na wanawake watatu wako mikononi mwa polisi kusaidia uchunguzi wa tukio hili la aina yake ambalo Mkuu wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Afande Charles Kenyela amethibitisha.


Pia Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mh. Jordan Rugimbana naye amethibitisha tukio hilo na kuahidi kulitolea ufafanuzi ofisini kwake kesho saa sita kamili mchana. Pichani juu ni sehemu ya miili ya vichanga hao ambayo haikuweza kuoneshwa yote kwa sababu za kimaadili



mama bishanga aongea leo dar



Mama Christina Innocent , jina la Usanii ni Mama Bishanga (kushoto) na kulia ni mwanae Hendrick Nambira, jina la Usanii Kenny akizungumza na Waandishi wa Habari ambao hawapo kwenye picha na kutoa ushauri kwa Wasanii wa Tanzania jinsi Filamu zinavyoendeshwa nchi nyingine,na kuwapongeza jinsi Watanzania walivyoendelea kwenye majukwa ya usanii, kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo) jijini Dar es Salaam leo. Picha na Anna Itenda -Maelezo.


Mama Bishanga ameongelea
mambo makuu matatu:



1. Umuhimu wa wasanii wa filamu na watendaji (wapiga picha, waongozaji, watu wa taa nk.) wafanye juu chini wasomee fani hiyo badala ya kutegemea uzoefu tu kwani bila weledi fani hio itadoda. Ameitaka serikali itoe kipaumbele mafunzo ya sanaa ya filamu kama zilivyo fani zinginezo.


2. Amesisitiza umuhimu wa uhalisia ambao unakosekana sana katika filamu za Tanzania kiasi nyingi zionaonekena kama maigizo yasiyo na mvuto. Amesisitiza umuhimu wa kuheshimu maadili ya nchi na kukataza kabisa waigizaji kucheza michezo ya ngono nje nje kwani hio si utamaduni wa mtanzania. Kuhusu filamu ya 'Shoga' inayozi9nduliwa wiki hii amesema ushoga si desturi ya Kitanzania na bila shaka filamu itapendwa kwani inatoa tahadhari ya tabia hio chafu. Ila amesema si vyema watu wakambeza mchezaji mkuu wa filamu hio kwa kudhani yeye ni shoga kweli, na kwamba huo sio ustaarabu kwani hata yeye aliwahi kusemwa mitaani na wenye uelewa mdogo kuwa ni mama mkatili baada ya kucheza kama mama mkwe mkatili.


3. Amewataka wasanii na wadau wa tasnia ya filamu kuendeleza libeneke kwani kazi zao zinaonekana na kuheshimika sana na kwamba wakiongezea weledi wa kwenda shule hakuna wa kuwagusa. Alimfagilia sana JK kwa kujituma kuendeleza michezo na sanaa, na kusema wasanii na wanamichezo wamuenzi Rais wetu kwa kujituma na kufanya vyema




madereva taxi na bodaboda wapewa somo na jeshi la polisi mkoani kagera


Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani Mkoani Kagera, Marson Mwakyoma (mwenye shati la drafti) akiwapa somo waendesha magari yanayobeba abiria wakati akitoa elimu kwa madereva kwa njia ya vitendo iliyotolewa na kikosi hicho jana kwa kushirikiana na Chuo cha Lake Zone kwenye viwanja vya Gymkana vilivyoko katika manispaa ya Bukoba, kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Chuo cha Udereva cha Lake Zone, Winston Kabantega na kulia kwake ni PC Mwinyi mkaguzi wa magari.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani Mkoani Kagera, Marson Mwakyoma akitoa elimu kwa njia ya vitendo kwa waendesha pikipiki zinazobeba abiria katika manispaa ya Bukoba, kushoto kwake ni Mkaguzi wa Magari wa Kikosi cha Usalama barabarani Mkoani Kagera, PC Alexander na mwenye suti ni Mkurugenzi wa Chuo cha Udereva cha Lake Zone, Wiston Kabantega, elimu hiyo ilitolewa kwenye viwanja vya Gymkana, elimu hiyo ni sehemu ya mikakati ya jeshi la polisi Mkoani Kagera ya kupambana na ajali mkoani Kagera.

washiriki wa shindano la kisura wa tanzania 2011 waanza kambi.


Pichani kati Mwenyekiti na Mwanzilishi wa mradi wa Kisura wa Tanzania (BTA), Juliana Urio,akizumgumza na baadhi ya waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusina kuanza kambi wa warembo wa shindano la Kisura wa Tanzania 20110.kushoto ni Meneja masoko wa SBC,Bwa.George Michael,Afisa Mipango Ujana wa FHI Bwa.Aziz Itaka,Mwisho kabisa ni Meneja Masoko wa ATCL,Bwa. Musyangi Kajeri
WAREMBO wanaowania taji la Kisura wa Tanzania 2010/11, wameingia kambini mapmea jana katika Hoteli ya Kiromo View Resort, iliyopo nje kidogo ya Mji wa Bagamoyo,Pwani, tayari kwa fainali zitakazofanyika Machi 12, mwaka huu. Kambi hiyo itahusisha wasichana 25 kutoka mikoa mbalimbali nchini, waliofanikiwakutinga katika hatua ya fainali za shindano hilo, baada ya mchujo uliofanyika kwa miezi miwili.

Mchakato wa kuwapata wasichana
hao, ulianza Desemba 11, mwaka jana, na kumalizika mapema mwezi wa kwanza, ukihusisha warembo kutoka mikoa ya Mwanza,Mara, Kagera, Shinyanga, Tabora, Dar es Salaam, Arusha, Manyara, Dodoma, Iringa,Mbeya na Ruvuma.

Akizungumza wakati wa kuwatambulisha warembo hao katika Hoteli ya Kiromo ViewResort, Mwenyekiti na Mwanzilishi wa mradi wa Kisura wa Tanzania, Juliana Urio kutoka kampuni ya Beautiful Tanzanie Agency (BTA), alisema kuwa warembo walioingia kambini, ni wale waliopita katika mchujo baada ya kukidhi vigezovinavyotakiwa.

Vigezo hivyo urefu wa sentimita174, mapaja 36, kiuno 25, kifua 36 na umri ni kati ya miaka 18-27, bila kujali kama mshiriki ameolewa, kuzaa au la.“Mwaka huu idadi ya warembo walioingia kambini imeongezeka, kutoka 20 kama ilivyokuwa awali hadi 25, hii ikitokana na mdhamini wetu Kiromo View Resort kutupa nafasi ya pekee ya kuongeza wasichana watano zaidi,” alisema.Urio aliwataja warembo walioingia kambini kuwa ni Neema Methew na Silipa Swai kutoka Mwanza, Lilian Bussa na Gaudencia Joseph (Mara), Beatrice James (Kagera),

Monica Fikiri na Angella Mombeki (Tabora).Wengine ni Suzana Manoko, Winnfrida Sabega, Rita Swai, Lethina Christoper, Joyce Joseph, Happiness Salimenya, Grace David (Dar es salaam), Dotinata Soro, Neema Kilango, Neema Seley (Arusha), Kipoyane Laibon (Manyara), Mariam-Kissa Isaack, Asha Hamisi, Flavian Makungwa, Lucy John (Dodoma) na Queen Kabisama (Ruvuma).

Alisema kuwa wakiwa kambini, warembo hao watapewa mafunzo mbalimbali kuhusiana na maisha yao binafsi na jinsi ya kukabiliana na changamoto zinazowazunguka katika maisha yao ya kila siku, ikiwa ni pamoja na kutembelea maeneo tofauti. Urio aliwapongeza warembo waliopata bahati ya kutinga fainali za shindano hilo,ikiwa ni pamoja na kuwashukuru wazazi waliowaruhusu watoto wao kujiunga shindano hilo, akiwaahidi ‘kuwapika’ vilivyo warembo hao ili waweze kuwa mfano wa kuigwa kwa jamii ya kitanzania kutokana na matendo yao.

Mdhamini mkuu wa shindano hilo ambalo linafanyika kwa mara ya tatu sasa, ni Family Health International (FHI), wakati wadhamini wengine ni TBC1, Kiromo View Resort, TanFoam (Arusha), SBC Limited, Flare Magazine, Hugo Domingo, BASATA, GRM Production, Clouds FM, ATCL na MJ Records

Local Lads To Take On Corporations In Indoor Cricket League


The Dar Businesmen's Dream Team
Some 15 Dar-es-Salaam businessmen have joined forces to take on corporate sponsored teams in the fast paced world of indoor cricket. The public is invited to show support for the Hennessy Hitters, captained by Kishen Savani, by coming to their opening match at Funkys Orbit (Masaki) on Monday the 31st January, at 9pm.


Hennessy embodies the values of creativity, innovation and the art of living (LVMH). In line with this philosophy, and impressed by the team’s community spirit, Hennessy offered its sponsorship. This is the story of the Hennessy Hitters.




“The team was formed by a group of friends who played cricket when we were younger. “ says Captain Savani. “We have been training hard over the past few weeks, we have a strong squad and we look forward to winning this opening match”.


The Hennessy Hitters team comprises of the following, Kishen Savani (Captain), Chintu Patel (Vice-captain), Kevin Patel, Nishit Kanabar, Imran Hirji, Heri Bomani, Nadir Hirji, Nitesh Patel, Prahlad Nathwani, Rupesh Kanabar, Situ Ramji, Akash Patel, Pullen Manek, Anand Patel and Gopal Patel.


“Through patronage, we wish to give something back that is in the general interest and thereby share our economic success with everyone.” – LVMH (Louis Vuitton • Moët Hennessy)


The next 5 matches will be played on:
31/1 at 2100 Hrs
3/2 at 1840, 8/2 at 2100 Hrs
10/2 at 1950 Hrs
and 18/2 at 1840 Hrs


Hennessy Hitters Shall play their First Match
Against a team named 'Not So Hot Chilies'.

ZAIDI YA WAGONJWA 263 WA FESTULA NA MDOMO WA SUNGURA WAMENUFAIKA NA HUDUMA YA M PESA


Mkurugenzi msaidizi wa hospitali ya CCBRT Haika Mawala akimkaribisha Mkurugenzi wa mahusiano na Vodacom Foundation Mwamvita Makamba wa pili toka kushoto akiambatana na Mkuu wa kitengo cha Safaricom Foundation-Kenya Sanda Ojiambo walipotembelea hospitali ya CCBRT kwa lengo la kujionea jinsi gani huduma ya Vodafone M pesa inavyosaidia wagonjwa wa fistula na mdomo wa sungura kwa kutumiwa fedha za nauli na matumizi ya njiani kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini na kuja kutibiwa hospitalini hapo zaidi ya wagonjwa 263 wamenufaika na huduma hiyo.
Mkurugenzi msaidizi wa hospitali ya CCBRT Haika Mawala akimkaribisha
Mkurugenzi wa mahusiano na Vodacom Foundation Mwamvita Makamba
Mkurugenzi wa Vodafone Foundation wa Egypt Noha Saad kushoto akisaini kitabu cha wageni katika hospitali ya CCBRT mara baada ya kutembelea hospitalini hapo na wakurugenzi wenzake Mwamvita Makamba,Mkuu wa kitengo cha Safaricom Foundation-Kenya Sanda Ojiambo wakiwa na lengo la kujionea jinsi gani huduma ya Vodafone M pesa inavyosaidia wagonjwa wa mdomo wa sungura na fistula kwa kutumiwa fedha za nauli na matumizi ya njiani kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini na kuja kutibiwa hospitalini hapo zaidi ya wagonjwa 263 wamenufaika na huduma hiyo.
Mkuu wa kitengo cha Safaricom Foundation-Kenya Sanda Ojiambo(kushoto)akizungumza na waandishi wa habari katika hospitali ya CCBRT walipotembelea hospitalini hapo kwa lengo la kujionea ni jinsi gani huduma ya M pesa inavyosaidia wagonjwa wa fetula na wa mdomo wa sungura kwa kutumiwa fedha za nauli na matumizi ya njiani kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini na kuja kutibiwa hospitalini hapo zaidi ya wagonjwa 263 wamenufaika na huduma hiyo,katikati Mkurugenzi wa Vodafone Foundation Uingereza Andrew Dunnet,Mkurugenzi wa Vodafone Foundation Tanzania Mwamvita Makamba.
Mkurugenzi wa hospitali ya CCBRT Tom Vanneste akifafanua jambo kuhusu ugonjwa wa mdomo kisungura na fistula kwa maafisa wa Vodafone M pesa Afrika walipotembelea hospitalini hapo hawapo pichani kujionea jinsi gani huduma ya M pesa inavyosaidia wagonjwa kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini na kuja kutibiwa hospitalini hapo zaidi ya wagonjwa 263 wamenufaika na huduma hiyo.


eXTReMe Tracker

1 comment:

Unknown said...

great post! I love your site. glad that you share it with everyone.urgent care

Umesoma hizi hapa