Promote your business for free grow your business for life you don't need to spend more money anywhere.

THIS BLOG IS SPONSORED BY AHADIWAY ,ADVANTAGES FOR JOINING AHADIWAY BOON CAREER (ABC) CHAPTER = Employment opportunities within and outside the country. , Job experience , Self -employment , Field stations, part time jobs and chances to be trained.

Tuesday, June 25, 2013

DAR DAMU TUPU



Na Waandishi Wetu  JIJI la Dar es Salaam wiki iliyopita lilikumbwa na

matukio ya kutisha yaliyosababisha lionekane ni la damu baada ya majambazi kufanya uhalifu 

wa kutisha sehemu mbalimbali kwa kuwapiga risasi watu huku wakipora

 fedha na mali.


 
 Zwahili Miraji.
Gazeti hili lilipita maeneo mengi na kubaini yafuatayo:
DENTI CHUO KIKUU ALIVYOMIMINIWA RISASI
Lilikuwa ni kundi la majambazi sita waliovamia Chuo Kikuu cha Dar es salaam

 usiku wa kuamkia Ijumaa iliyopita na kufanikiwa kuwapora wanafunzi
 waliokuwa wakijisomea vitu kadhaa na kummiminia risasi mmoja wao.
Tukio hilo la kusikitisha lilitokea saa 9.00 usiku katika ukumbi ujulikanao

 kwa jina la Yombo 1 ambapo mwanafunzi Alex Robert, 26, alipigwa risasi.
Kwa mujibu wa taarifa za kiuchunguzi, majambazi waliingia katika ukumb

i huo wakiwa  na silaha za jadi pamoja na bunduki aina ya shortgun.


Samwel Michael.
Chanzo makini cha gazeti hili chuoni hapo kilisema kuwa 




majambazi hayo yalipofika ukumbini yaliwaamuru wanafunzi hao kulala
 chini na kukabidhi kila walichokuwa nacho, amri ambayo wanafunzi hao
 walitii kwa kuwapa kompyuta mpakato, simu na fedha.
Hata hivyo, mwanafunzi mmoja aliamka na kuwaomba wamrejeshee flashi

 yake, ambapo jambazi mmoja aliichomoa na kumtupia ndipo Alex 
alipoomba kurudishiwa kitambulisho kwa madai kuwa asingeweza
 kuingia ndani ya chumba cha mtihani bila kuwanacho.

Alex Robert.




























 Kitendo cha kuomba kitambulisho ndiyo chanzo cha kupigwa risasi mwanafunzi huyo 
wa kitivo cha sheria.
Mwanafunzi huyo alipigwa risasi mbele ya wenzake Joseph Hansi, Lunura Masalu 

na Kitojo Karani na baada ya tukio hilo wanafunzi hao walimchukua mwenzao na 
kumpeleka kituo cha afya chuoni hapo na baadaye alikimbizwa katika Hospitali ya
 Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Mara baada ya kitendo hicho, baadhi ya wanafunzi waliandamana kuelekea Kituo

 cha Polisi Chuo Kikuu kutaka msaada zaidi baada ya kuona askari walioajiriwa na
 chuo hawakutokea kupambana na wahalifu hao.
Wanafunzi waliliambia gazeti hili kuwa kwa hivi sasa usalama wa maisha na mali 

zao unatia shaka kutokana na askari wa chuo kutowajibika ipasavyo.















































eatus Kisanga.


“Siku ya tukio Ukumbi wa  Yombo 1 haukuwa na mlinzi yeyote hadi
tulipoomba msaada kutoka polisi makao makuu, huu ni uzembe,
” alisema mwanafunzi mmoja kwa sharti la kutotajwa jina gazetini.
Makamu Mkuu wa Chuo,Utawala, Yunus Mgaya aliliambia gazeti 

hili kuwa uongozi wa chuo hicho unasikitishwa na tukio hilo na
 akaahidi kuimarisha ulinzi.
Afisa Habari Mkuu wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,  Aminieli

  Aligaeshi alisema mwanafunzi huyo amefanyiwa upasuaji na
 kutolewa risasi tumboni na hivi sasa yuko chini ya uangalizi wa
 madaktari katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU).
Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, CP Suleiman

 Kova amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na akasema majambazi
 hayo yalikuwa na silaha ikiwemo bunduki na upelelezi unaendelea.
Akizungumzia maandamano yaliyotokea chuoni hapo alisema:

 “Wanafunzi chuoni hapo walikuwa na lengo la kushinikiza ulinzi.
 Jeshi la polisi kanda maalum kwa kushirikiana na  makamanda 
wa mikoa wanaendelea na msako mkali dhidi ya wahalifu hao.”

MFANYABIASHARA APIGWA RISASI, APORWA
Wakati huohuo, Ijumaa iliyopita saa 8 mchana majambazi yakiwa

 na pikipiki na bastola yalimpiga risasi na kumpora kiasi kikubwa 
cha fedha wakala wa magazeti ya makampuni mbalimbali nchini.
Wakala huyo aliyejulikana kwa jina la Zwahili Miraji Mrutu akizungumza 

na gazeti hili akiwa Hospitali ya Muhimbili alisema, alikuwa maeneo ya
 mitaa ya Kipata na Swahili jijini Dar akiwa anapeleka fedha benki ghafla 
alijikuta akipigwa risasi kifuani na kuporwa pesa.
 Akizungumza kwa shida katika Wodi ya Kibasila, Mrutu alisema: 

“Majambazi hayo yalikuwa na pikipiki na wakaniambia niwape fedha
, nilipozing’ang’ania, walinipiga risasi moja kifuani na mbili hewani
 kwa lengo la kutawanya watu.”
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Ilala, ACP Marietha Minangi

 alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.
“Tukio hilo kweli limetokea na majeruhi huyo yupo katika Hospitali

 ya Taifa Muhimbili akiendelea na matibabu huku nasi tukiendelea 
na upelelezi,” alisema Kamanda Minangi.

ANYONGWA KIKATILI
Naye mwendesha pikipiki ya miguu mitatu maarufu kama Bajaj amb

aye kituo chake kilikuwa maeneo ya Sayansi, Beatus Kisanga, mkazi
 wa Makumbusho, Dar, ameuawa kinyama kwa kunyongwa na kamba
 na majambazi.
Tukio hilo lilitokea ndani ya Baa ya Serengeti iliyopo maeneo hayo

 huku kaka yake ambaye ni mlinzi wa baa hiyo aitwaye Batlista Kisanga
 alikutwa akiwa hoi hajitambui.
Akizungumza na Uwazi, mmiliki wa baa hiyo, Venancy Lyimo alisema

 kuwa marehemu aliuawa saa 11 alfajiri naye alipewa taarifa hizo kwa
 njia ya simu na kijana ambaye anafanya usafi mishale ya saa moja asubuhi.
“Kijana huyo aliniambia kuwa alimkuta mlinzi  akiwa kaunta hajitambui

 huku vinywaji vikiwa vimetolewa nje na kuzagaa chini. Nilitoka nyumbani
 kuja hapa kazini,” alisema.
Aliongeza kuwa baada ya kufika alimkuta marehemu akiwa amefungwa 

kamba mikononi na miguuni huku mdomoni amefungwa kitambaa na
 mwili wake ukiwa umetupwa kwenye jiko la kuchomea nyama.
“Kinachoonekana ni kwamba wale majambazi waliwapa sumu hawa jamaa

,’’ alisema Lyimo.
Aliongeza kuwa, aliwapigia simu polisi waliofika na kuuchukua mwili wa 

marehemu huku mlinzi akipelekwa Hospitali ya Mwananyamala kwa
 matibabu.
Kaka wa marehemu aitwaye Yesse Peter akizungumza na Uwazi, alisema 

kwamba mwili wa marehemu ungesafirishwa wakati wowote kwenda 
Mbeya kwa mazishi.

KACHERO WA POLISI ANUSURIKA KUUAWA
Wakati hayo yakitokea, askari wa upelelezi aliyefahamika kwa jina la

 Samwel Michael usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita alinusurika
 kuuawa na wananchi waliomhisi kuwa ni jambazi baada ya kupata 
ajali ya bodaboda.
Askari huyo alihisiwa na wananchi kuwa ni muhalifu baada ya kukutwa 

na bastola huku akiwa amepoteza fahamu.
Tukio hilo lilitokea karibu na Kituo cha Drive Inn, Msasani jijini Dar 

ambapo mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo alisema: “Nilianza kupata 
mashaka baada ya kumuona jamaa akiendesha pikipiki aina ya Bajaj
 Boxer kwa kasi.
“Nikiwa namshangaa ghafla nilimuona akilivaa hili greda ambalo

 limeegeshwa hapa baada ya kumaliza kufanya ukarabati wa hii barabara.”
Akiwa eneo la tukio mwandishi wetu alimshuhudia askari huyo akitapatapa

 kutaka kuamka huku baadhi ya wananchi wakisema huenda ni 
jambazi na kutaka kummaliza.
Wakati wananchi hao wakitaka kummaliza ghafla alitokea askari wa

 kikosi cha usalama barabarani na kuchukua bastola iliyokuwa
 pembeni ya majeruhi huyo na kuanza kumpekua.
Baada ya kumkagua alimkuta na kitambulisho chake cha kupigia 

kura pamoja na cha kazi kilichoonesha alikuwa  askari wa upelelezi 
pia alimkuta na pingu pamoja na nyaraka zingine.
Baada ya kupata vielelezo hivyo afande huyo aliwaondoa hofu wananchi

 waliokuwa wakitaka kummaliza majeruhi huyo na kuwaambia kuwa 
 alikuwa ni askari wa upepelezi aliyekuwa kazini.
Baada ya kutulizwa wananchi hao waligeuka wasamaria wema na kuanza

 kumsaidia majeruhi huyo mpaka walipofika askari wengine ambao 
walimuwahisha hospitali kupata matibabu.

No comments:

Umesoma hizi hapa