Promote your business for free grow your business for life you don't need to spend more money anywhere.

THIS BLOG IS SPONSORED BY AHADIWAY ,ADVANTAGES FOR JOINING AHADIWAY BOON CAREER (ABC) CHAPTER = Employment opportunities within and outside the country. , Job experience , Self -employment , Field stations, part time jobs and chances to be trained.

Tuesday, June 25, 2013

INASIKITISHA MAMA ALIA BAADA YA KUJIFUNGUA MAPACHA WALIOUNGANA KWENYE MAKALIO MKOANI MBEYA...!


MWANAMKE mmoja mkazi wa Kijiji cha Kasumuru, Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya, 
 Grace Joel Lwesha (19), amelia baada ya kujifungua watoto walioungana.Akizungumza
 na waandishi wetu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Jengo la Watoto, Grace 
alilia kutokana na kile alichodai kujifungua watoto walioungana wakati yeye
 ni maskini. Watoto hao mapacha wa kiume, Eliudi na Elikana wameungana
 sehemu ya makalio hivyo kulazimika kutumia sehemu moja ya haja kubwa.

Grace aliwaambia waandishi wetu kwamba, watoto hao walizaliwa katika
 Hospitali ya Kyela, Februari 20, mwaka huu wakiwa na miguu miwili na
 mikono miwili kila mmoja.
“Baada ya kujifungua Machi mosi nilihamishiwa katika Hospitali ya 
Mkoa wa Mbeya kwa uchunguzi zaidi ili waweze kujua ni jinsi 
gani watakavyotenganishwa,” alisema.
Hata hivyo, hospitali hiyo ya mkoa haikufanikiwa badala yake Machi 16, 
walimhamishia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo kuanzia 
hapo mpaka sasa anafanyiwa maandalizi kwa ajili ya safari ya kupelekwa
 nchini India kwa upasuaji.
 “Ninawapenda sana watoto wangu hawa pamoja na kwamba wapo
 katika hali hii, ndugu zangu walipokuja hospitalini kuniona akiwema
 mama yangu walinifariji na kunisihi nisiwachukie nizidi kuwapenda.
“Kuwatunza ni kazi ngumu sana kwani mara nyingi wamekuwa 
wakininyima usingizi kwa sababu wamekuwa wakilala kwa nyakati tofauti.
“Nakumbuka siku niliyojifungua mume wangu alikosa raha lakini sasa
 anawapenda kwani amejua kuwa hii ni zawadi kutoka kwa Mungu.

 “Maisha yetu ni magumu kwani tunatoka kwenye familia maskini,
 kazi yetu ni kilimo cha kutumia jembe la mkono hivyo bado kuna mahitaji 
mengi nashindwa kumudu. Nichukue nafasi hii kuwaomba msaada 
Watanzania wote walioguswa na tukio hili,” alisema Grace.
Grace alifunga ndoa na Erick William Mwakyusa Desemba 23, 2010 na 
katika ndoa yao wamejaliwa kupata mtoto mmoja aitwaye Lide (3) na hao
 mapacha ni uzao wake wa pili.
Mama huyo anaomba msaada kwa mtu yeyote aliyeguswa na habari hii
 atume mchango wake kupitia namba 0753308525 ambayo ni ya 
mumewe au aende kumuona Muhimbili.






No comments:

Umesoma hizi hapa