Promote your business for free grow your business for life you don't need to spend more money anywhere.

THIS BLOG IS SPONSORED BY AHADIWAY ,ADVANTAGES FOR JOINING AHADIWAY BOON CAREER (ABC) CHAPTER = Employment opportunities within and outside the country. , Job experience , Self -employment , Field stations, part time jobs and chances to be trained.

Wednesday, July 4, 2012

HATIMAYE ALBINO ALIYEUWAWA MIEZI MIWILI ILIYOPITA AZIKWA ARUSHA..PICHA



MAZISHI YAKIENDELEA 
WAOMBOLEZAJI WAKIWA MBELE YA KABURI LA MAREHEMU HUYO 





MRATIBU WA POLISI ARUSHA, HAMIS WARIOBA

Na Idd Uwesu/Mpwaji Arusha yetu

Hatimaye mazishi ya mtu mwenye ulemavu wa ngozi aliyeuwa kinyama wilayani Arumeru mkoani Arusha miezi miwili iliyopita yamefanyika katika makaburi ya Njiro jijini Arusha.

Mazishi ya mlemavu huyo ambaye hakuweza kutambuliwa kutokana na kuchunwa ngozi na kuondolewa baadhi ya viungo vyake yamefanyika chini ya usimamizi wa Chama cha Maalbino Tanzania TAS na Shirika la Under the same sun Tanzania
Mwanahabari wetu Idd UWESU anataarifa zaidi.

Akiongea wakati wa mazishi hayo Mkurugenzi wa shirika la Under the same sun Tanzania, Vicky Ntetema amesema kuwa jukumu la kuwalinda walemavu wa ngozi nchini ni jukumu la kila mmoja na sio kuliachia jeshi la polisi pekee au serikali. Amesema jamii ihakikishe walemavu hao wanalindwa na kuthaminiwa kama binadamu wengine.


Ameongeza kuwa mauaji hayo ya kinyama ni lazima yakomeshwe na kwamba wale wote waliohusika na unyama huo kuhakikisha wanakamatwa na kufikishwa mbele ya sheria. Amesema jamii ya kitanzania haina budi kuhakikisha inashirikana na jeshi la polisi kuhakikisha watu hao wanakamatwa.

Insert 1……Mkurugenzi UTSS Tanzania, Vicky Ntetema


Nae mwenyekiti wa mkoa wa Chama cha Maalbino Tanzania, Godson Mollel amesema wanalaani vikali tukio hilo na kuitaka serikali na mashirika mengine kukisaidia Chama chao ili kiweze kutembea maeneo mengi zaidi kuendelea kuelimisha jamii hasa za vijijini kuhusu imani hizo potofu ambazo ndizo chanzo kikubwa cha mauaji hay

Insert 2……Mwenyekiti TAS Arusha, Godson Mollel.

Kwa upande wa Jeshi la polisi, Mrakibu wa Polisi mkoa wa Arusha Hamis Warioba amesema Jeshi hilo hivi sasa linaendelea na uchunguzi na kwa mba halitasimama mpaka lihakikishe watu waliohusika na mauaji hayo wanakatamatwa na kufikishwa mbele ya sheria.

Insert 3……. Mrakibu wa Polisi mkoa wa Arusha, Hamis Warioba

Mwili wa mlemavu huyo uliokotwa tarehe 29 mwezi mei mwaka huu pembezoni mwa nyumba ya mkazi mmoja wilayani Arumeru. Mazishi hayo pia yalihudhuriwa na Mariamu Staford mlemavu wa ngozi ambaye alikatwa mikono yake alipovamiwa na watu wasiojulikana nyumbani kwao huko Ngara.CREDITS: ARUSHA 

No comments:

Umesoma hizi hapa