Promote your business for free grow your business for life you don't need to spend more money anywhere.

THIS BLOG IS SPONSORED BY AHADIWAY ,ADVANTAGES FOR JOINING AHADIWAY BOON CAREER (ABC) CHAPTER = Employment opportunities within and outside the country. , Job experience , Self -employment , Field stations, part time jobs and chances to be trained.

Sunday, June 24, 2012

MIMBA YA LULU YATOKA


Na Shakoor Jongo
ULE ujauzito wa miezi mitatu wa mwigizaji nyota wa sinema Bongo ambaye kwa sasa yuko nyuma ya nondo za Gereza la Segerea, Dar es Salaam kwa kesi ya kifo cha Steven Kanumba, Elizabeth Michael 'Lulu' umedaiwa kuchoropoka, Ijumaa Wikienda lina cha kushika mkononi.
CHANZO CHAFUNGUKA
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika ambacho ni makini, sababu kubwa ya mimba hiyo kutoka ni kutunga nje ya mfuko wa uzazi hali ambayo ingemletea matatizo Lulu.
“Nikwambie kitu, unajua wengi wanaamini Lulu ana mimba na hivi karibuini iliandikwa imefikisha miezi mitatu, ilikuwa sahihi, lakini ukweli ni kwamba kwa sasa imetoka.
“Sababu kubwa ni kwamba afya yake ilidorora, ukiachia ule ugonjwa wa U.T.I alioripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba anao, lakini kingine ni kuwa iligundulika ujazuito wake ulitunga nje ya mfuko wa uzazi ikawa haina jinsi, ikabidi kutolewa na kusafishwa,” kilisema chanzo hicho bila kuainisha tukio hilo lilitokea lini.
ETI NI MIMBA YA TATU
Kikiendelea kuzungumza kwa umakini mkubwa, chanzo chetu kilidai kuwa eti ujauzito huo ni wa tatu kuchoropoka kwa msanii huyo.
“Unajua huu unakuwa ujauzito wa tatu kwa Lulu kutoka. Kwa kweli kama si hivyo angekuwa na mtoto,” kilisema chanzo bila kuweka wazi nyingine mbili zilitoka kwa matatizo gani.
“Kuna wakati Lulu alikwenda China, aliporudi alikuwa na ujauzito, lakini nao ulitoka, inaonekana ana matatizo kidogo kwenye upande wa kizazi,” kilidai chanzo hicho.
Kikaendelea: “Baada ya hapo, haukupita muda mrefu, akanasa nyingine ya mwanamuziki mmoja wa Bongo Fleva, pia hiyo nayo ikaja kutoka ya tatu ni hii ya Kanumba.”
MAMA LULU
Katika kupata mzani wa habari hiyo, Ijumaa Wikienda lilimsaka mama Lulu, Lucresia Karugila ili kusikia kutoka kwake lakini hakupatikana hewani kutokana na kuzima simu.
USHUSHUSHU GEREZANI
Ijumaa Wikienda lilituma ‘mpelelezi’ wake kwenye Gereza la Segerea ili kukutana na Lulu na kuzungumza naye kuhusu madai ya mimba yake kuchoropoka.
Ilikuwa kazi kubwa kumpata ‘laivu’ nyota huyo kutokana na ukweli kwamba kuna watu maalum watatu ambao ndiyo wenye ruhusa ya kumwona mtuhumiwa huyo, mbali na hao marufuku kwa wengine.
Hata hivyo, ‘shushushu’ huyo alifanikiwa kupata fursa ya kumjulia hali mahabusu mwingine aliyepo kwenye gereza hilo na ndipo akapata bahati ya kuonana na Lulu ambaye alionekana kuwa mnyonge.
Baada ya salamu, shushushu wetu alimuuliza Lulu kuhusu afya yake na ya ujauzito alionao ambapo alijibu kwa mkato.
“Nani amekwambia mimi nina mimba?”
MASTAA WA BONGO WANENA
Baadhi ya mastaa wa sinema Bongo ambao hawakuwa tayari majina yao kuchorwa gazetini, walipozungumza na gazeti hili kuhusu kuwepo au kutokuwepo kwa ujauzito wa Lulu walipishana ‘kiswahili’.
Wapo waliodai ujauzito huo ulitoka akiwa gerezani, wengine walidai ulitoka wiki moja kabla ya kifo cha Kanumba lakini wapo waliodai bado anao.
Staa wa kiume: “Lulu hana ujauzito, ulitoka. Ninavyojua mimi, wiki moja kabla ya kifo cha marehemu (Kanumba) ndiyo ulitoka, kwa hiyo hana.”
Staa wa kike: “Lulu bado ana mimba ila ni siri sana. Lakini hata nyiye wenyewe si mmeona tumbo lile, anao.”
Staa wa kike: Lulu mpaka anaingia kwenye matatizo kwa kifo cha Kanumba alikuwa na kibendi, hawezi kukitoa kwa sasa, maana yuko gerezani.”
Lulu anatarajiwa kufikishwa Mahakama Kuu ya Tanzania Mei 28, mwaka huu ili kujibu tuhuma zinazomkabili juu ya kifo cha Kanumba.

No comments:

Umesoma hizi hapa