Promote your business for free grow your business for life you don't need to spend more money anywhere.

THIS BLOG IS SPONSORED BY AHADIWAY ,ADVANTAGES FOR JOINING AHADIWAY BOON CAREER (ABC) CHAPTER = Employment opportunities within and outside the country. , Job experience , Self -employment , Field stations, part time jobs and chances to be trained.

Monday, May 28, 2012

Mapishi ya Vitumbua




Baada ya kumiss vitafunio vya nyumbani nikaamuua kupika vitumbua.

Recipe ya vitumbua vyangu nikama ifuatavyo:


  • Unga wa mchele ( Vikombe 2 vikubwa)
  • Sukari (Nusu ya kikombe kikubwa)
  • Hamira ( Nusu ya kijiko cha chai)
  • Hiliki (Nusu ya kijiko cha chai)
  • Tui la nazi ( Kikombe kimoja kikubwa)
  • Unga wa ngano (Vijiko viwili vya chakula)
  • Mafuta ya kuchomea (Vegetable oil)
Matayarisho

Unachanga unga, sukari, hamira, hiliki, unga wa ngano na tui la nazi pamoja katika bakuli la plastiki. Kisha unaukoroga mpaka mchanganyiko unakuwa kama uji mzito. Kava bakuli lililokuwa na mchanganyiko kisha hifadhi katika sehemu yenye joto kwa muda wa masaa matatu. 

Jinsi ya kupika

Weka chuma cha kuchomea vitumbua katika moto wa wastani, kisha weka mafuta kwenye chuma cha kuchomea ( Kijiko kimoja cha chai) mafuta yakisha pata moto tia uji wako (upawa mmoja) katika kila shimo la chuma cha kuchomea. Acha mpaka kitumbua kikauke kisha geuza na tia mafuta. Acha upande wa pili wa kitumbua mpaka uwe rangi ya kahawia na hapo kitumbua kitakuwa kimeiva utakitoa. Rudia hatua hizo kwa vitumbua  vyote vilivyobaki.

No comments:

Umesoma hizi hapa